• Home
  • About

Christian bella asema yeye sio msanii wa Bendi wala Bongo flavour...

Mwanamuziki Christian Bella amedai utakuwa unamkosea ukimwita yeye ni msanii wa muziki wa bendi au msanii wa muziki wa bongofleva kwa kuwa anafanya muziki wa aina nyingi.


Mkali huyo wa masauti ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Nishike’, ameiambia Bongo5 kuwa yeye ni mwanamuziki kwa kuwa anafanya vitu vingi ndani ya muziki.
“Mimi ni msanii ninayefanya muziki ndani ya Tanzania, sio muziki wa bongofleva, sio muziki wa dansi, sio msanii wa taarabu,” alisema Bella “Mimi ni mwanamuziki, mimi ni mwanamuziki kwa ujumla, usiniseme mimi ni Bella msanii wa muziki wa dansi au Bella msanii wa muziki wa bongofleva au Bella msanii wa taarab au Bella msanii wa R&B, Christian Bella ni mwanamuziki,”
Aliongeza “Mimi nafanya muziki kufurahisha kila mtu, nafanya muziki kufurahisha wanahip hop, wana bongofleva, wana dansi,wana taarab ndio maana mimi naitwa mwanamuziki,”
Pia muimbaji huyo amewataka mashabiki wa muziki wake kukaa makao wa kula kwa ajili ya ujio wa studio yake pamoja na label ya kusimamia wasanii.
  
CREDIT: BONGO5

Post a Comment

LEAVE YOUR COMENT HERE...