Diamond hakwenda Las Vegas kutumbuiza tu bali pia ameitumia fursa
hiyo kumalizia kiporo cha wimbo wake na Ne-Yo. Wawili hao walirekodi kwa
mara ya kwanza wimbo wao mwaka jana jijini Nairobi lakini kuna vitu
hawakumalizia.
Diamond, Ne-Yo, Babutale na producer Jesse Corporal Wilson
Akiwa Las Vegas, staa huyo aliingia studio na Ne-Yo pamoja na producer, Jesse Corporal Wilson aliyeshiriki kutayarisha nyimbi nyingi za Ne-Yo.
Huenda pia akatumia fursa hiyo kufanya video ya wimbo huo.
Pia staa huyo alikutana na rapper na muigizaji wa Empire, Bryshere Y.
Gray aka Yazz The Greatest anayejulikana kwenye tamthilia hiyo kwa jina
la Hakeem.
Credit: Bongo5
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...