• Home
  • About

Diamond aingia studio kumaliza wimbo na Ne-Yo, akutana na Hakeem wa Empire

Diamond hakwenda Las Vegas kutumbuiza tu bali pia ameitumia fursa hiyo kumalizia kiporo cha wimbo wake na Ne-Yo. Wawili hao walirekodi kwa mara ya kwanza wimbo wao mwaka jana jijini Nairobi lakini kuna vitu hawakumalizia.

12677509_902198513229954_1033016786_n
Diamond, Ne-Yo, Babutale na producer Jesse Corporal Wilson
Akiwa Las Vegas, staa huyo aliingia studio na Ne-Yo pamoja na producer, Jesse Corporal Wilson aliyeshiriki kutayarisha nyimbi nyingi za Ne-Yo.
Huenda pia akatumia fursa hiyo kufanya video ya wimbo huo.
12093519_195637737469802_552226387_n
Pia staa huyo alikutana na rapper na muigizaji wa Empire, Bryshere Y. Gray aka Yazz The Greatest anayejulikana kwenye tamthilia hiyo kwa jina la Hakeem.

Credit: Bongo5

Post a Comment

LEAVE YOUR COMENT HERE...