Msanii Baraka da Prince siku za nyuma aliwahikutangaza ujio wa collabo zake na wasanii kadhaa kama Eddy Kenzo wa Uganda na Patoranking wa Nigeria lakini
hazikuwahi kutokea.
Muimbaji huyo wa ‘Siwezi’ amedai sababu za kutofanyika kwa collabo hizo ni kwasababu alibadilisha uongozi wake
“Ni kweli Collabo zilitakiwa zifanyike lakini sema baada ya kuwa
na uongozi mpya sikuweza kufanya collabo na Eddy Kenzo na Patoranking
hiyo ndio ilikuwa sababu kubwa na kila kitu kilikuwa kimefanyika
kilichobaki ni mimi tu kufanya nao sema kilichosababisha ni kuwa na
uongozi mpya kwani uongozi wa zamani ndio walikuwa wamepanga collabo
hizo”
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...