Beki wa kati wa timu ya Azam FC, Aggrey Morris amefurahi kurudi tena
uwanjani baada ya kuumia goti na kukaa nje ya uwanja takribani miezi
mitatu.
Morris ambaye aliumia akiwa na timu ya taifa ya Zanzibar amesema
alikuwa akiumia kuwa nje wakati timu yake ilihitaji msaada wake.
Akiongea na mtandao wa timu hiyo, Aggrey Morris alisema, “Nafurahi
sana kurejea dimbani tena, nilikuwa natamani sana kucheza, kuna muda
nilikuwa naumia sana nilipokuwa naona timu yangu inahitaji msaada wangu
na mimi pia nilikuwa natamani kuisaidia, sisi wachezaji tunapenda
kucheza, nilihisi kuna kitu naweza kuisaidia timu yangu kwa hiyo
nafurahia kurejea na najua nitatoa mchango kwa timu yangu.”
“Mimi nawaambia mashabiki waendelee kuwa nami, kwa sababu najua
walimiss kwa kipindi kirefu na wamenivumilia kusema kweli na
wamenisapoti kwa kipindi chote kigumu pia watarajie tu kujitoa kwa moyo
wangu wote kuisaidia timu yangu,” alimalizia Morris,” aliongezea Morris.
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...