Baada ya kudumu kwa kipindi cha miaka 19, kundi la P-Square
limevunjika rasmi. Hakuna aliyewahi kuwaza iwapo kundi hili maarufu na
lililofanikiwa kuliko yote Afrika lingeweza kufika katika hatua hii.
Ni hatua iliyowashtua wengi. Kwa sasa Paul na Peter Okoye ni wasanii
wawili wanaojitegemea. Paul aka Rudeboy ameanzisha record label yake,
Rudeboy Records, na Peter aka Mr P ametangaza rasmi uongozi wake mpya.
Nini chanzo cha ugomvi wao?
Inaonekana kuwa ugomvi ndani ya kundi hili ulikuwepo kwa muda mrefu
na kwa kiasi kikubwa ulitokana na kaka yao Jude, kuwa meneja wao. Peter
alihisi uongozi wa kaka yake uliokuwa wa kifamilia zaidi ulikuwa hauko
sawa na alihitaji mabadiliko.
“A manager is been employed by the artiste not the other way round. #truthBeTold,” aliandika Peter February 17 mwaka huu katika mfululizo wa tweets kuelezea matatizo yao.
“People change management and you r not different. Usher Raymond
did it,BeyoncĂ© did it as well. So it’s not new. Peter and Paul have the
right to sack the entire management team. Business is Business. #Period.
Been nurturing and managing these problems for over 4yrs now. Don’t
take my silence as a weakness. #done,” aliongeza.
Mwanzoni alipigania kundi lao lisife lakini uongozi ubadilike.
“What the fans want is Peter and Paul Psquare and that’s what I
want. Period! Psquare is not breaking up. But the management needs to
go.”
Lakini inaonekana kuwa Paul hakuwa tayari kumtoa kaka yao Jude kama
meneja wao. Na hiyo ndiyo sababu Peter ameamua kujiondoa kwenye kundi
hilo. Mapacha hao walijikuta wakigawanyika na kurushiana vijembe
February 18 kwenye Instagram. Paul alipost picha ambayo awali ilikuwa
ikiwaonesha wao na kaka yao Jude, lakini akamuondoa Peter na kuandika:
This is where I belong and this is where I stand…….you do music
in the studio, not on social media, you have family issues, you discuss
that in close doors, not on social media ….. Family is family, blood is
blood …. If you don’t do family business, then who am I to you?”
Kitendo hicho kilimuumiza Peter aliyejibu: And cutting me off
from a picture and replacing me with a studio set says it all my bro.
All because you want to sound matured and letting the pple insult and
Laff at me. Peter Okoye the social media rant. I wish you well in all
you do my bro. God bless our hustle.”
Mama yao angekuwepo yasingetokea?
Paul anaamini kama mama yake angelikuwa hai, yote yanayoendelea yasingetokea.
“Wish you were around, now I understand what these life is
without having a mother, you’ve played your part thank you very much
mum, miss you,” aliandika Paul kwenye picha ya marehemu mama yao aliyoiweka Instagram.
Mashabiki wameuamia lakini inabidi waukubali ukweli kuwa kundi hilo
lililoiteka Afrika kwa kishindo kwa takriban miongo miwili limevunjika.
Na sasa Peter na Paul wanaanza maisha ya solo huku Peter tayari akiwa
ameanza kufanya show zake mwenyewe. Nani atafanya vizuri zaidi ya
mwenzake? Muda utaongea.
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...