Mtandao wa Ghafla Kenya umeripoti kuwa, baada ya kudumu na Lebo yake
kubwa ya muziki Kenya, Grand Pa Records Rapa DNA ameamua kumaliza
mkataba na lebo hiyo na kuamua kuchukua njia yake.
Katika taarifa yao kupitia vyombo vya habari, Grand Pa Records
wamesema kuwa mkataba wao na mwanamuziki huyo ulimalizika rasmi Mei
mwaka huu ambapo pande zote mbili yani wao na DNA hawakuwa na nia ya
kuendelea tena kufanya kazi pamoja hivyo kulazimika kutosaini mkataba
mwingine.
DNA akiwa pamoja na Record Lebo hiyo alitoa ngoma kali zilizotamba
Afrika Mashariki ikiwemo Banjuka ambayo ilimuweka kwenye ramani nzuri
hivyo kwa yeye kuondoka na kuacha kufanya kazi na Grand Pa kumeibua hali
ya wasiwasi juu ya mustakabali wa muziki wake miongoni mwa mashabiki
lakini hawakusita kumtakia mema aendako.
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...