• Home
  • About

Rapa DNA ame amua kumaliza mkataba na Grand pa Records

 Mtandao wa Ghafla Kenya umeripoti kuwa, baada ya kudumu na Lebo yake kubwa ya muziki Kenya, Grand Pa Records Rapa DNA ameamua kumaliza mkataba na lebo hiyo na kuamua kuchukua njia yake.
Katika taarifa yao kupitia vyombo vya habari, Grand Pa Records wamesema kuwa mkataba wao na mwanamuziki huyo ulimalizika rasmi Mei mwaka huu ambapo pande zote mbili yani wao na DNA hawakuwa na nia ya kuendelea tena kufanya kazi pamoja hivyo kulazimika kutosaini mkataba mwingine.


DNA akiwa pamoja na Record Lebo hiyo alitoa ngoma kali zilizotamba Afrika Mashariki ikiwemo Banjuka ambayo ilimuweka kwenye ramani nzuri hivyo kwa yeye kuondoka na kuacha kufanya kazi na Grand Pa kumeibua hali ya wasiwasi juu ya mustakabali wa muziki wake miongoni mwa mashabiki lakini hawakusita kumtakia mema aendako.

Post a Comment

LEAVE YOUR COMENT HERE...