“Watu wengi wamekuwa wakisema wamechoka kila siku kuona majengo ya Dar
es Salaam, kwa hiyo tumeamua kubadilika kuja huku halafu Mwanza yenyewe
sio town ni kidogo nje ya mji. Nafikiri kutokana na mandhari ya Mwanza
mawe mawe mtu atakuwa anajua kabisa kwamba project imefanyika ndani ya
Rock City.” Amesema Hemedy.
Ameelezea kuwa filamu hiyo inahusu
vijana wawili ambao walikuwa wameenda kijijini kwa lengo la kutafuta
vijana wanaojua kuigiza ili wawaunganishe na wasanii wakubwa wa mjini
lakini mwisho wa siku vijana hao wageuka na kuendekeza uzinzi na kuwa
wezi.
Vijana hao waliishia kwenye mikono ya wanakijiji waliowashambulia kwa kipigo kikali baada ya kukamatwa wakiiba kuku.
Amesema
lengo la kuigiza filamu hiyo ni kufikisha ujumbe kwa wasanii wenzao
kuwa kama wanaamua kusaidia watu wafanye hivyo na si vinginevyo.
“Kwa
hiyo ni kuwafungua macho wale wote wanaotumika kwa style hiyo, na
vilevile kuonesha wasanii kwamba kama tunaamua kusaidia tusaidie kweli
na isiwe watu tunawafanyia michezo mibaya kama hiyo.”
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...