Kiswahili kimetumika kwenye episode ya kwanza ya msimu wa pili wa
tamthilia ya Quantico ulioanza kuoneshwa Jumapili kupitia runinga ya ABC
ya Marekani.
Kinasikika baada ya kundi la watu waliokuwa wamevaa mask kuvamia
mkutano ambao Rais wa Marekani alikuwepo pamoja na mke wake. Watu hao
wanajiita Citizens’ Liberation Front na wanatumia Kiswahili kuwasiliana.
Msimu wa pili unaendelea kuangalia harakati za kishujaa za wakala wa
FBI, Alexandra “Alex” Parrish, nafasi inayochezwa na Priyanka Chopra.
Kwenye msimu wa pili yumo staa wa Afrika Kusini, Pearl Thusi anayetumia jina Dayana Mampasi kwenye tamthilia hiyo.
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...