Msanii wa muziki, Lady Jaydee amekutana na Ray C hivi karibuni na kumshauri mambo kadhaa kuhusu afya yake.
Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo wake wa Ndindindi,
ameonyesha kutoridhika na afya ya Ray C na kuamua kumwandikia ujumbe wa
kumpa matuamaini.
Kupitia instagram, Jay Dee ameandika:
A message of Hope: Kila mtu anapitia magumu katika
maisha kwa njia tofauti hakuna jaribu lisilo na mlango wa kutokea.
Amini na amua nakupa moyo na Mungu akusaidie kwa yote unayopitia
akuondolee akuepushie na akupe kufahamu na kukiri mabaya.
Watu wanakupenda nakumbuka tulivyoanza kimtindo nai miss competition pls
Come Back naamini bado unayo nafasi . Binti amka jikaze anza mwendo,
umrembo na bado wang’ara . Ni baada ya miaka 6 tangu kuonana mara ya
mwisho, story nazo ni ndefu na nyingi
Ombi:
Tuheshimu na kuhurumia matatizo ya wengine, tafadhali msi comment vibaya wala kwa kejeli.
Lolote linaweza kumfika yoyote
Saa yoyote
Tuonyeshe Mapenzi
#PowerOfPositivity
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...