Rappper kutoka TipTop Connection,Dogo Janja amekanusha kuandikiwa
nyimbo na rapper Darasa.Hatua hiyo imekuja ikiwa ni siku moja tangu
Darasa kudai kuwa anajuta kumuandikia Janjaro track inayofahamika kama
“Ya Moyoni”,kwani licha ya kutolipwa,ilimsababishia lawama kati yake na
baadhi ya watu.
“Sijawahi kuandikiwa nyimbo na Darasa,wala hatukuwahi kuwa na
makubaliano yeyote ya yeye kuniandikia nyimbo,tulikua studio pamoja ni
kama alikua akinipa idea tu lakini ngoma niliandika mwenyewe”aliongeza
Janjaro.
Kuhusu tetesi za kutokua na maelewano mazuri na Paka rapper Young
Dee,rapper huyo anaefanya vizuri na ngoma yake ya “My Life”,amedai hana
ugomvi na Young Dee kama baadhi ya watu wanavyodhani na hategemei kuwa
na ugomvi na msanii yeyote.Teamtz.com ilipomuuliza kama yupo tayari
endapo ikitokea Young Dee anataka kufanya collbo na yeye,Janjaro alijibu
“mpaka sasa nina collbo mbili tu,na kama ikitokea nafanya collabo
ntafanya collabo na wasanii wenye future,sio tu kufanya
collabo,nafikiria kufanya collbo na mtu mwenye mipango”Janjaro alijibu.
Credit:teentz
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...