CEO wa WCB Wasafi, Diamond Platnumz ametangaza rasmi kumtambulisha msanii mpya wa label yake baada ya mafanikio makubwa ya Harmonize.
Diamond alitoa taarifa hiyo kupitia twitter.
Pia Diamond alifafanua zaidi kwa kuandika ujumbe mwingine kupitia ukurasa wa instagram.Panapo Majaaliwa Jumatano Hii Wcb_Wasafi tutamtambulisha rasmi Kijana Mwingine Mpya…tafadhali wadau tunaomba sana Support zenu…🙏— Chibu Dangote (@diamondplatnumz) March 14, 2016
“Wengi wetu tumezaliwa katika familia duni na ndiomaana kidogo tunachokipata ni vyema kukitumia kusaidia wenzetu ili nao kesho wawainue na wengine… tafadhali wadau tunaomba sana mtusaidie kuwasupport vijana wenzetu…..Maana Sisi wenyewe kwa wenyewe ndio wakunyanyuana 🙏 #BADO,” aliandika Diamond.
Label ya Wasafi ina wasanii wawili, Harmonize pamoja na Raymond.
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...