Nakala za filamu mpya ya JB na Wema Sepetu, ‘Chungu Cha Tatu’
zilizoingia sokoni Jumatatu hii zimemalizika ikiwa ni siku tatu toka
iachiwe.
JB alisema kasi ya mauzo ya filamu hiyo, ina kila dalili ya kuvunja rekodi ya filamu yake iliyopita Mzee wa Swagga.
“Filamu
inaenda vizuri sana, Jumatatu baada ya kuingia sokoni masaa manne kopi
zilizoingia sokoni ziliisha, Jumanne tukazalisha tena zikaisha, leo hii
tumezalisha nyingine nyingi kwa sababu hata mikoani nilipigiwa simu
kwamba zimeisha. Kwahiyo nashukuru mashabiki kwa kuonesha kuniunga
mkono,” alisema JB.
JB alisema filamu hiyo imemgharimu takriban shilingi milioni 68 mpaka kukamilika.
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...