Sheddy amesema kuwa sababu kubwa inayowafanya wasanii wengi wa Hip Hop kutomfata kufanya naye kazi ni kutokana na kuwa wanamskia akitengeneza zaidi kazi za wasanii wa kuimba.
Amewataja wasanii wa Hip Hop ambao anatamani kufanya nao kazi kuwa ni Joh Makini na Fid Q.
“Natamani sana kufanya kazi na msanii kama Joh Makini, Fid Q” alisema Sheddy
“Lakini unajua inakuwa ngumu kwasababu gani unajua, wanaona tutaenda vipi kwa Sheddy jamani kila siku tunasikia tu ngoma ngoma za kuimba wabana pua, kwahiyo wanakuwa wanakosa ule moyo.”
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...