Kama una mfollow Ben Pol kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii basi umeshakutana na picha akiwa ughaibuni, yuko nchini Ujerumani
na ameeleza kilichompeleka huko.
Ben Pol na Emanuel Austin
Hit Maker wa ‘Sofia’ Ben Pol amesema kuwa ameenda Ujerumani kushiriki
katika utengenezwaji wa video ya Mtanzania Emannuel Austin aishiye
huko, ambaye alimshirikisha Ben Pol kwenye wimbo wake alipotembelea
Tanzania mwaka jana.
Ben Pol akiwa onset na warembo wa Kijerumani
“Kimsingi nipo nchini Ujerumani Frankfurt, niko na mshikaji wangu
mmoja anaitwa Emanuel Austin, ni choreographer ni muimbaji ambaye asili
yake ni Tanzania lakini yuko based nchini Ujerumani. Mwaka jana
alikuwepo Tanzania nilirekodi nae wimbo kwenye studio za Authentic,
lakini beat ilifanywa na Fundi Samweli. Kwahivyo sasa hivi tunafanya
music video huku Ujerumani tunafanya na the number one producer wa music
video huku Ujerumani.” Alisema Ben Pol kupitia 255 ya Clouds Fm.
Usikilize wimbo wa Emanuel austin akiwa na Ben Paul... Ukiwa na jina Ruka.
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...