Hii ni mara ya pili Williams anapata kitu kutoka kwa Cee-Lo sababu pia amechukua nafasi yake kama kocha mpya wa season ya saba kwenye mashindano ya kuimba ya The Voice.
Kabla ya noma yake “Happy” phareel alikua ni Producer na mwimbaji ambae amewahi kuingia kwenye headlines za chati za muziki duniani kwa single kama kolabo na Snoop Dog na Jay Z na amewahi kuwaandikia nyimbo wakali kama Kanye West, Gwen Stefani, Gloria Estefan.
Pamoja na kwamba Pharrell alimuandikia Michael Jackson hizo nyimbo hizo anasema timu yake ilizikataa, yani timu ya MJ ilizikataa hata baada ya Michael Jackson kuzipenda na kuzikubali nyimbo hizo baadae.
‘Nimefanya nyimbo nane kwa ajili ya Michael lakini zote hazikumfikia na ziliishia kurekodiwa na Justin Timberlake lakini baadae Michael mwenyewe aliniimbia hizo nyimbo na kusema zilitakiwa ziwe zake na nikamjibu kuwa zilikua za kwako’
CREDIT | Millardayo.com
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...