Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete akizungumza na Wahariri wa baadhi ya vyombo vya habari usiku wa juzi,
Jumatano, Aprili 16 katika mahojiano maalum ya kuadhimisha Miaka 50 ya
Muungano, Rais Kikwete amesema: kuwa ni utovu wa
nidhamu na ukosefu wa adabu, kwa baadhi ya Wa Tanzania kuwatukana,
kuwadhihaki na kuwakejeli Waanzilishi wa Taifa la Tanzania, Hayati Julius Nyerere na Hayati Sheikh Abeid Amaan Karume.
Rais Kikwete amesema kuwa viongozi hao wawili wameifanyia Tanzania
mambo mengi makubwa na ya kihistoria, kiasi cha kwamba Watanzania wanao
wajibu wa kudumisha na kuenzi heshima yao kwa namna ya kudumu.
Rais Kikwete ametoa msimamo huo baada ya kuwa ameulizwa kuhusu matusi,
kejeli, dhihaki ambazo zimekuwa zinaonyeshwa na wajumbe wachache wa
Bunge Maalum la Katiba juu ya waasisi hao wa Tanzania na Wabunifu Wakuu
wa Muungano wa Tanzania.
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...