Drake na Rihanna wanaendelea kushibana na penzi lao linachanua huku wakiripotiwa kuwa na mpango wa kuishi pamoja kama mume na mke.
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Star la America, chanzo kimoja kimeeleza kuwa
Drake amemnunulia Rihanna zawadi ya pete ya almasi yenye rangi ya njano
yenye thamani ya $42,000 (sawa na 68,712,000/-).
Hata hivyo imeelezwa kuwa pete hiyo sio ya uchumba.
“Rihanna aliikubali zawadi hiyo kama ishara ya mapenzi ya Drake. Sasa
hivi (Drake) anabadili hata ratiba zake ili atumie muda mwingi ipasavyo
kuwa na Rihanna.” Kilieleza chanzo hicho.
Drake na Rihanna wanaonekana kuwa karibu zaidi kadiri siku
zinavyozidi kwenda, na hata Jumapili katika MTV Movie Awards walionekana
wakiwa wameshikana mikono muda mfupi baada ya Drake kuperform.
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...