Bunge maalum la katiba leo April 25 linahairishwa bila kupitisha
ibara hata moja kati ya 240 ambazo zimo katika rasimu ya katiba bunge
hili linahairishwa mpaka mwezi Agosti mwaka huu huku likiendelea
kujadili sura ya kwanza na ya sita yenye jumla ya ibara 19 zinazohusu
masuala yanayojega msingi wa aina ya muungano unayopendekezwa.
Tume ya mabadiliko ya katiba katika rasimu ya katiba iliyowasilishwa
bungeni na aliyekua Mwenyekiti wake Jaji Warioba ilipendekezwa muundo
wenye shirikisho la serikali 3,pendekezo ambalo bado limeleta mtafaruku
bungeni baada ya kutengeneza pande mbili bungeni kutokana na mgawanyiko
huo kauli zenye utata,kejeli,matusi,dhihaka na ubaguzi ni mambo
yanayojitokeza sana kwenye sura hizo mbili.
Miongoni mwa vitu vinavyolaumiwa kwa bunge hili la katiba ni matumizi
ya lugha zisizofaa kwenye uchangiaji bila kujali kuwa bunge hilo
linatazamwa na watu wa rika mbalimbali.
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...