Muongozaji wa video ama director Nisher ameeleza jinsi alivyofanya kazi kupita
kiasi ndani ya mwaka 2013/2014 hali iliyomsababisha kupoteza fahamu na
kukimbizwa hospitali.
Nisher ambaye kwa sasa yupo mapumziko, amekiambia kipindi cha Mkasi
cha EATV kuwa, hali hiyo ilisababisha familia yake imshauri apumzike.
“Nilikuwa nafanya kazi sana kuanzia mwaka 2012, 2013 mpaka 2014 mpaka
kuna kipindi nilizimia nikiwa naedit video. Nikaanguka chini next time
naamka nakuta nipo hospitali nimetundukiwa drip naambiwa ulizimia. Kwa
sasabu I was working too much ili kuprove watu wanachotaka,” alisema.
Aliongeza,”Kwa mfano sasa hivi sitoi tena kazi nipo break, this
industry ina tendency ya kukufanya ujisikie, ujione yaani kuna wasanii
wengi ambao wakishafaulu wanaanza kuwaangalia wenzao kama hawana kitu
chochote. So nikaanza kuona kama naanza kufika hicho kipande na kama
nakinusa hivi so nikawa mwepesi hivi kustep down.”
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...