Ikiwa ni wiki chache zimepita toka aachie wimbo/video mpya ‘Nana’ ,
Diamond ametua jijini Lagos, Nigeria alikoenda kufanya promo zaidi ya
wimbo huo aliomshirikisha msanii wa huko.
Diamond Platnumz akiwa ameongozana na team yake wakiwemo mameneja
wake Salaam na Babu Tale, pamoja na Dj wake Romy Jons, ameenda nchini
Nigeria kufanya media tour ya kuitangaza ngoma yake mpya
aliyomshirikisha Flavour.
“Ofcourse am in Town already…. shukran sana #CocaCola kwa
kuniwezesha kwenye safari hii ya kuja kuitandaza vyema #Bongoflavour
yetu #LAGOS #IAmAreason Cc @romyjons @iam_kcee @salaam_sk”-alipost Diamond
Msanii Kcee wa Nigeria ambaye pia ametoa wimbo aliomshirikisha
Diamond hivi karibuni ‘Love Boat’, ndiye ameonekana kuwa mwenyeji wao
toka walipowasili uwanja wa ndege.
“Chilling with my peps @diamondplatnumz@babutale @romyjons @iamharrysong Live in Lagos” – alipost Kcee kwenye moja ya picha.
Siku chache zilizopita Diamond alifanya media tour nyingine Afrika
Kusini kutangaza collabo mpya aliyofanya na msanii wa huko, Donald
ambayo video yake pia imefanyika wiki iliyopita.
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...