• Home
  • About

Papa francis kufanya maombi pamoja na Maraisi wa Israel na Palestina.

Kiongozi wa kanisa Katoliki duniani, Papa Francis amewapokea rais wa Israel, Shimon Pez na rais wa Palestina, Mahamoud Abbas katika makao makuu ya kanisa hilo Vatican kwa lengo la kufanya maombi maalum ya kuombea amani ya mashariki ya kati.
Walikutana na papa nje ya makaazi yake na baadae kuungana na kiongozi wa kanisa la Ordhodoz, Partriarch Artholomew kwa hafla maalum.

Papa alizungumza katika hafula hiyo fupi:
“Kuleta amani kunahitji ujasiri mkubwa kuliko vita. Kunahitaji ujasiri wa kusema ndio kwa mkutano na La kwa vita; ndio kwa mashauriano na La kwa makabiliano; ndio kwa kuheshimu mikataba na La kwa uchokozi; Ndio kwa ukweli na La kwa Uongo; kwa haya yote tunahitaji ujasiri na nguvu moyoni.”
Maombi ya imani ya Kiislamu na imani ya Kikristo yatafanyika Vatican  ikiwa ni mara ya kwanza maombi na mafundisho ya Quran kufanyika hapo.

Post a Comment

LEAVE YOUR COMENT HERE...