• Home
  • About

Mwanzilishi wa Instagram kuwa shughulikia wanao weka picha chafu.

 Mtandao wa kijamii wa Instagram umezidi kuwa maarufu kutokana na jinsi ambavyo unampa nafasi mtumiaji kuionesha dunia taswira yake binafsi au hata kuhusu hisia zake.

Hata hivyo watu mbalimbali wamekuwa wakipost picha tata za nusu utupu na nyingine zikipitiliza kitu ambacho mwanzilishi wa Instagram, Kevin Systrom hakiafiki kabisa na amekivalia njuga kukikomesha.
Akiongea na mtandao wa BBC Newbeat, Kevin amesema kampuni yake imepiga marufuku na haitaruhusu picha za aina hiyo kwa kuwa wanahitaji mtandao huo kuwa salama na rafiki kwa watu wa rika zote (wakubwa na watoto).
Kevin amefanya mahojiano na mtandao huo baada ya Scout Wills,  mtoto wa kike wa mcheza filamu maarufu, Bruce Wills kupinga hatua ya Instagram kuondoa picha yake aliyo aliyoweka huku matiti yakiwa wazi.
Rihanna ambaye aliwahi kupewa onyo na Instagram kwa picha alizokuwa anaweka, alimsapoti Scout kabla hajaamua kujitoa siku iliyofuata.

Post a Comment

LEAVE YOUR COMENT HERE...