• Home
  • About

VIDEO | Mwana ume mmoja nchini Kenya ajichimbia kaburi nakujizika kisa kikiwa mapenzi.

 MWANAUME AJICHIMBIA KABURI KISA MAPENZI

Kituo cha runinga cha KTN nchini Kenya kimesema tukio hilo lililotokea Jumanne asubuhi na kuwashangaza wakazi wa eneo la Trans Nzoia mkoa wa Rift Valley. Mwanaume huyo anayetambulika kwa jina la Kipsang, alidai kuwa ana matatizo ya ndoa ambayo yeye mwenyewe ameshidwa kuyatatua na kwa hivyo kwake kilichosalia ni kwenda mbinguni. Alisema mkewe alikuwa amemwambia jambo ambalo lilimkera roho na ndio maana akaamua kujitoa uhai. Mwanaume huyo alichimba kaburi hilo usiku na hata kujaribu kujizika akiwa hai wakati mkewe na watoto wake walipokuwa wanalala.
Wanakijiji katika kijiji cha Tivani walikuwa na wasiwasi kuwa mwanamume huyo alikuwa amerukwa na akili ingawa walikiri kwamba yeye na mkewe wamekuwa wakikumwba na matatizo ya ndoa. Mkewe alisema kuwa amechoshwa na mwanamume huyo ambaye ametelekeza familia na majukumu yake. Baba huyo wa watoto wawili ambaye ni kondakta wa matatu, hatimaye aliondoka katika kaburi hilo baada ya wanakijiji kumsihi huku wazee wakiwataka watu kupanda migomba ya ndizi eneo alilokuwa amechimba kaburi hilo ili kuzuia mikosi.

Post a Comment

LEAVE YOUR COMENT HERE...