Kituo cha runinga cha KTN nchini Kenya kimesema tukio hilo
lililotokea Jumanne asubuhi na kuwashangaza wakazi wa eneo la Trans
Nzoia mkoa wa Rift Valley. Mwanaume huyo anayetambulika kwa jina la
Kipsang, alidai kuwa ana matatizo ya ndoa ambayo yeye mwenyewe ameshidwa
kuyatatua na kwa hivyo kwake kilichosalia ni kwenda mbinguni. Alisema
mkewe alikuwa amemwambia jambo ambalo lilimkera roho na ndio maana
akaamua kujitoa uhai. Mwanaume huyo alichimba kaburi hilo usiku na hata
kujaribu kujizika akiwa hai wakati mkewe na watoto wake walipokuwa
wanalala.
Wanakijiji katika kijiji cha Tivani walikuwa na wasiwasi kuwa
mwanamume huyo alikuwa amerukwa na akili ingawa walikiri kwamba yeye na
mkewe wamekuwa wakikumwba na matatizo ya ndoa. Mkewe alisema kuwa
amechoshwa na mwanamume huyo ambaye ametelekeza familia na majukumu
yake. Baba huyo wa watoto wawili ambaye ni kondakta wa matatu, hatimaye
aliondoka katika kaburi hilo baada ya wanakijiji kumsihi huku wazee
wakiwataka watu kupanda migomba ya ndizi eneo alilokuwa amechimba kaburi
hilo ili kuzuia mikosi.
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...