Kampuni
ya Bia Tanzania inayotengeneza kinywaji cha Kilimanjaro lager, leo hii
inakutana na waandishi wa habari kuzungumzia mwenendo wa mchakato wa
kuwapata washindi wa tuzo za muziki Tanzania, Kilimanjaro Tanzania Music
Awards 2014, mchakato ambao unaendelea kwa mwezi huu mzima kwa njia ya
watanzania kupiga kura.
Meneja wa Kinywaji cha Kilimanjaro, Bwana George Kavishe amewataka
watanzania kuendelea kupiga kura kwa wingi katika siku 6 zilizobakia,
ili kukamilisha asilimia 70 walizopewa kuchagua ni msanii gani
anayestahili kuchukua tuzo kwa mwaka huu.
Bwana Kavishe amesema kuwa, asilimia 30 zilizobaki katika kuamua
washindi, zitaamuliwa na timu ya majaji itakayoundwa na wadau wa chati
za muziki na wataalam, wakizingatia vigezo ambavyo vitawekwa wazi na
BASATA hivi karibuni.
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...