Baadhi yetu hatuwezi kukubali, ukweli kuwa mapenzi ndiyo yanaendesha
dunia, kwani hata Ali Kiba ana kibao chake kinachoukubali ukweli huu
kwamba mapenzi yana-run dunia.
Katika baadhi ya mahusiano ya kimapenzi, wapo wanaochokana haraka
kiasi cha kumshangaza mmoja wa wahusika, awe mwanaume au mwanamke,
ingawa uzoefu unaonyesha akina baba wengi ndiyo wenye tabia ya kukinai
mapema.
Wanaanza kwa kasi na nguvu kubwa, wakipiga simu kila baada ya muda
mfupi na sms kila dakika, lakini wakishafanikiwa kukutana kimwili na
mwenzake mara moja au mbili, taratibu ukaribu unaanza kuota mbawa,
mithili ya mapenzi ya miaka sita au saba iliyopita.
Hali hii inakuwa zaidi kwa wanaume, kwani ikishatokea wamekutana na
mwenza wake zaidi ya mara moja, wanaanza kupoteza spidi ya mwanzo, huku
baadhi yao wakileta dharau na sababu zisizo maana katika kuhalalisha
tabia yao mpya.
Hivi karibuni mwanamke mmoja msomaji wa safu hii, alinilalamikia juu
ya tabia ya mpenzi wake aliyekuwa akimsumbua sana mwanzoni, lakini sasa
mwanaume amebadilika kabisa baada ya kukutana naye mara tatu faragha.
Nilijitahidi kumpatia ushauri ambao naamini utamsaidia, lakini hapo
hapo nikapata wazo la kuandika mada hii hapa nikiamini itawasaidia wengi
pia kwa kuzingatia hali hii wanakutana nayo wanawake wengi. Zifuatazo
zaweza kuwa sababu zinazochangia hali ya mwanaume kupotea haraka mara
baada ya kufanikiwa kukutana kimwili na mwenza wake.
HANA MAPENZI YA DHATI
Kuwa makini, siyo kila anayetamka neno I love you anamaanisha. Wengi
wanatawaliwa na tamaa ya kingono tu na hawana mapenzi ya dhati. Na wengi
wa wanaume wapya unaokutana nao, wana wapenzi wao tayari.
Ndiyo maana wanaume wengi wa aina hii, wanakimbilia kutaka kukutana
kimwili na ili wafanikiwe katika hilo, watatumia kila aina ya mbinu
wanazozijua. Unapokutana na wa aina hii, jipange, usije kutafuta wa
kumlaumu. Kwa ujumla, akina kaka wa aina hii ni wenye kuongozwa na uchu
wa kimwili.
UJUZI FARAGHA
Sayansi na teknolojia zimeleta mambo mengi. Siku hizi watu wanaangalia
mitindo ya mapenzi mitandaoni. Wanatamani kukutana na wanachokiona
kutoka kwa wapenzi wao. Hivyo wanapokosa, nao hupoteza hamu.
KUTOTIMIA KWA MATARAJIO
Wapo wanaoanzisha uhusiano wa kimapenzi na mtu wakitegemea kufaidika kwa
kitu flani, kama vile mabadiliko ya maisha yao na kadhalika, hivyo
inapokuwa tofauti, hujiondoa mapema.
MAZOEA
Tatizo hili mara nyingi linawakuta akina dada. Wakishakuwa na mtu kwa
muda mrefu huchukulia kuwa ni mazoea na hivyo kufanya wanavyotaka bila
kujua kuwa wanawaudhi wenza wao, ambao ili kujiweka sawa kiakili huamua
kusaliti na au kusababisha dharau baina yao.
KUTOJALI
Hii zaidi ipo kwa wanaume, pale mwanzo walikuwa wakijali kwa kusikiliza
na kutimiza shida za wenza wao, lakini baada ya kupata walichohitaji,
hawana tena ‘mzuka’. Jambo hili huwakera wenza wao na kujikuta wakiamua
kukata mawasiliano mapema.Ushauri ni kwa wote, wake kwa waume, kila
mmoja kuwa chachu ya ustawi wa penzi, badala ya kusubiri kufanyiwa
unachotaka!
MAZINGIRA
Hii ni moja ya sababu ambayo pia inasababisha wapenzi wengi kuchokana
haraka. Utakuta wapenzi wamezoea kukutana faragha chumbani tu hakuna
hata siku moja ambayo wanabadilisha mazingira
Wapenzi wanatakiwa kubadilisha mazingira kwani wasipofanya hivyo,
hata akili huwa inachoka na hii haimaanishi labda muende hotelini,
inawezekana hamna uwezo huo, basi fanyeni mabadiliko ya mazingira
hukohuko nyumbani kwenu, yaani mnabadilisha maeneo, kama leo mlizungumza
mkiwa sebuleni, basi kesho mfanye hivyo mkiwa kwenye kochi na siku
nyingine mnaweza kushusha godoro chini!
MAWASILIANO
Mawasiliano ni kitu muhimu sana katika mapenzi. Katika ulimwengu wa leo
hakuna mapenzi kama hakuna mawasiliano.Hapa ninazungumzia wapenzi
kuwasiliana kama kupigiana simu, kutumiana meseji za kuulizana
umeshindaje, umekula, kazi na mengine mengi, hii ni kinga tosha ya
kutochokana haraka, hivyo hata kama uko bize kiasi gani jitahidi
kuwasiliana na umpendaye.
Wapo wapenzi ambao wanapitisha hata siku mbili au tatu bila
kuwasiliana na wenza wao wakati mwanzoni mwa penzi lao haikuwa hivyo,
walikuwa wanatumiana meseji au kupigiana simu kila wakati lakini siku
zinavyokwenda ndivyo mawasiliano yanakuwa hafifu au unakuta mmoja yaani
mwanamke au mwanaume ndiye anayejitoa kila wakati kujitahidi kuwasiliana
na mwenzake, lakini mwisho anachoka na penzi linaishia hapo maana
hakuna thamani au wanajikuta wanatafutana pale mmoja anapokuwa na
uhitaji wa kimwili, haya siyo mapenzi.
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...