Marehemu
George Tyson aliye kua muongozaji wa filamu na vipindi vya Television mwili wake utaagwa kesho (June3) katika viwanja vya leaders Club, Dar
es Salaam na kisha kusafirishwa kwenda kwao nchini Kenya kwa maziko.
“Tunashukuru Mungu mwili wa George Tyson umewasili jana Dar es salaam
ukitokea mkoani Morogoro na mwili umehifadhiwa katika hospitali ya
Kairuki, kumuaga marehemu itakuwa Leaders Club siku ya Jumanne na baada
ya kuuaga mwili utasafirishwa Kenya kwa mazishi.” Mwenyekiti wa Bongo
Movies, Steve Nyerere ameiambia Bongo5.
Marehemu George Tyson Otieno, alifariki katika ajali ya gari iliyotokea katika
eneo la Gairo, Morogoro alipokuwa akitokea Dodoma na timu ya The Mboni
Show kutoa msaada wa madawati kwa shule moja ya msingi na walikuwa njiani
wakirudi jijini Dar es Salaam.
Katika gari hilo alilokuwemo marehemu Tyson na watu wengine nane na
yeye pekee ndiye aliyepoteza maisha huku wengine wakijeruhiwa..
Post a Comment
LEAVE YOUR COMENT HERE...